Social Icons

Loading...

ABDI KASSIM BABI STAA WA KIMATAIFA NA TAIFA STAR ATUA NCHINI...JE KAJA KUUENDELEA NA LIGI YA NYUMBANI?NA KAMA NI HIVYO TIMU GANI ANAJIANDAA KUINGIA...SOMA HAPA...

November 11 millardayo.com ilifanya exclusive interview na kiungo wa kimataifa waTanzania anayecheza soka la kulipwa Malaysia katika klabu ya UiTM Abdi Kassim Sadallah ambaye amewahi kutamba katika vilabu kadhaa vya Ligi Kuu soka Tanzania bara ikiwemo YangaAzam FC pamoja na Mtibwa Sugar.
Abdi Kassim ambaye pia anafahamika kama Babi au Ballack wa Unguja anacheza katika klabu ya UiTM inayomilikiwa na University of Technology MARA cha Malaysiaamemaliza mkataba na klabu hiyo aliyojiunga nayo mwaka 2014 hivyo amegoma kuongeza mkataba mpya kwanza akitafakari ofa aliyopewa.
IMG-20151111-WA0006
 Kiungo huyo ambaye bado yuko Malaysia licha ya kuwa Ligi Kuu imemalizika huku yeye akiwa kacheza mechi zote 22, kufunga magoli 7 na kuisaidia klabu yake UiTM kumaliza nafasi ya 8 katika msimamo wa Ligi Kuu Malaysia, bado hajakubali kuongeza mkataba mpya na klabu hiyo kutokana na timu hiyo kutofikia dau analolitaka hivyo bado anatafakari ofa hiyo hadi mwezi January au February 2016 au anaweza kutimkia Indonesia.
IMG-20151111-WA0024
Kiufupi Ligi imemalizika na mimi mkataba umemalizika kwa hiyo sasa hivi ninachoangalia connection tofauti tofauti hapa Malaysia na Indonesia kwa hiyo sasa hivi nipo likizo nategemea kuja Tanzania kuona familia lakini nina mipango ya kurudi Malaysia January au February nitarudi tena kuendelea na soka au naweza kwenda Indonesia” >>> Abdi Kassim

author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright MAWINGUBONGO
Back To Top